• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

Katibu wa CCM asisitiza kutumia majina ya waasisi kwenye mashindano Kilombero

Posted on: November 9th, 2019

Pichani juu: Katibu mkuu wa CCM Dr. Bashiru Ally akizungumza na Wananchi

KATIBU Mkuu Wa Chama Cha Mapinduzi(Ccm) Taifa Dk Bashiru Ally amepiga marufuku mashindano yanayoandaliwa na viongozi Wa kuchaguliwa kuitwa majina yao na badala yake kutumia majina ya waasisi Wa taifa hili.

Akizungumza na wanaCcm katika mkutano wake uliofanyika Jana uwanja Wa Tangani mjini Ifakara,Dk Bashiru alisema haileti picha nzuri kwa kipindi hiki Mbunge ama Diwani kuandaa mashindamo mbalimbali, akitumia jina lake na hii itaonyesha ameanza kujinadi kabla ya muda.

"Mashindano yanaweza tumika vibaya hasa wakati huu kuelekea ktk udiwan, ubunge na urais kuwa ni sehemu ya kujinadi kabla ya muda,hivyo tutumie majina ya waasisi wetu ili kuondoa mgangano huo,"alisisitiza.

 Bashiru ametoa kauli hiyo baada ya Mbunge Wa Viti maalum Mchungaji Dk Getrude Rwakatare kumueleza kuwa, toka ateuliwe na Rais Dk Magufuli amefanya mambo mengi, ikiwamo kuwaunganisha Vijana katika mashindano maalum aliyoyaandaa, yaliyokuwa yakijulikana kwa jina la Rwakatare Cup.

Aidha Amesema kuwa, licha ya mashindano hayo kumalizika, ila kwa sasa Mbunge huyo akitaka kuanzisha mashindano mengine, itabidi atumie jina la Kawawa na mashindano yatajulikana kwa Kawawa Cup badala ya Rwakatare Cup.

Amebainisha kuwa kwa kipindi hiki kuelekea uchaguzi mwakani hapendi kuona mwanaCcm akimlalamikia mwanaCcm mwenzie eti amecheza rafu kwa kujinadi kabla ya muda kufika.

"Wapo wenye nia wanaweza ogopa kwa kuona baadhi wanafanya mambo kama hayo kwani uzani unaweza usiwe sawa kwa wananchi na wanaccm,"alisema.

Amewataka wana Kilombero waendelee kutembea kifua na kuchapa kazi kwani taifa linawatambua kwa uzalishaji mzuri Wa zao la mpunga na kudai kwa sasa nchi ina chakula kingi cha kutosha.

Pia amewataka wananchi kuacha kugombana kwa sababu ya vyama vya siasa na kusema kuwa vyama visiwe chanzo cha kututenganisha bali vitumike kutuunganisha.

Kuhusu uandikishaji Wa wanachama wapya,Dk Bashiru aliwataka viongozi kuanzia ngazi ya shina hadi wilaya kuendelea zoezi la uandikishaji na waache tabia ya kudai kwanza Fedha ya kadi na kusema wawasajili kwanza na Fedha kuchukua baadae.

Awali Mbunge Wa Viti maalum Mchungaji Dk Gertrude Rwakatare amesema toka awamu ya tano iingie madarakani, kumekuwa na mabadiliko makubwa katika sekta mbalimbali.

Dk Rwakatare amesema nae toka ateuliwe amezunguka majimbo yote mawili, na kutoa misaada mbalimbali ndani ya chama na serikalini ikiwemo kutoa mikopo kwa akina mama, kugawa kadi za Ccm kwa wanachama wapya zaidi ya 70,000 na kutoa baiskeli 300 kwa makatibu Wa Kata na matawi Wa Ccm.

Nae Mwenyekiti Wa Ccm Wilaya ya Kilombero Clarence Mgomba alisema kuwa, Wilaya ipo vizuri kwa sasa kwani ushirikiano baina ya chama na watendaji Wa halmashauri zote ni Mkubwa.

Amemshukuru Rais kwa kuwapatia halmashauri Mbili za Mlimba na Ifakara na kumuahidi kuwa mwaka 2020, hawatakuwa na Mbunge Wa kuteuliwa bali watakuwa na wabunge Wa kuchaguliwa katika majimbo yote mawili.

Matangazo

  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOFAULU NA KUCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 18, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOFAULU MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2019 HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOMBERO December 09, 2019
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 15, 2020
  • FURSA KATIKA SEKTA YA KILIMO March 27, 2017
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Halmashauri ya wilaya ya Mlimba yakadiria bajeti yake

    January 25, 2021
  • Madiwani sikilizeni wananchi: DC Mlawa

    December 19, 2020
  • maafisa kilimo wekeni malengo

    November 27, 2020
  • Mhandisi Kalobelo azindua msimu mpya wa kilimo 2020/2021 Wilayani Mlimba ,azitaka Halmashauri kuimarisha vyama vya ushirika.

    November 27, 2020
  • Angalia zote

Video

MAKAO MAKUU KILOMBERODC KUHAMIA MNGETA
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa